Wednesday 25 January 2012

MAMBO YA JIKONI: VIAZI MASALA

Mahitaji:
Viazi mviringo
Nyanya ya kopo
Vitunguu swaumu
Ndimu
Chumvi
Mafuta ya Kupikia
Pilipili Manga
Methi
Spices zozote za chakula uzipendazo


Jinsi ya Kuandaa
Menya viazi. Vioshe na vichemshe. vikiiva viepue, visiive sana maana vitapondeka pondeka wakati wa kupika, na kupoteza maana halisi ya chakula.
Menya na kutwanga vitunguu swaumu vyako, viwe vingi ndio vinaleta ladha ya chakula hiki . Weka mafuta, weka vitunguu swaumu ongeza methi na viungo vyako unavyotumia kuongeza ladha ya chakula. Vikishakua vya brown weka  nyanya ya kopo, weka na maji kidogo ili kutengeneza roast nzito, weka pilipili mtama, ndimu na chumvi . Sasa weka viazi vyako huku unakoroga mpaka viazi vyako vipate roast. wacha vichemke kidogo.Chakula kitakua tayari kwa kuliwa.


                                      Chakula hiki kinaweza kuliwa mkate, au chapati. 

2 comments:

Thank you for visiting our website

Wazoefu Computer Technology

Search This Blog

Please Share This

Thanks for Like and Tweet